Thursday, March 13, 2014

SERIKALI YAJIPANGA KUWA NA SERA YA FILAM

Serikali ya Tanzania imejipanga kuendeleza
kwa dhati TASNIA ya Filamu ili kuwa chanzo
kikubwa cha ajira kwa wasanii na pia
kuongeza uchumi wa nchi .
Ni dhahiri kuwa sekta ya filamu ni njia
madhubuti ya kutambulisha jamii
kiutamaduni, kisiasa na kijamii na pia
katika kukuza na kuongeza fursa za nchi
katika uwekezaji na utalii.
Filamu na Makala za Filamu zikitumika
vizuri zitaweza kuhamisha na kuondoa
tofauti mbalimbali zilizopo ndani ya jamii
na hivyo kuongeza umoja na mshikamano
baina ya watu wa makabila na watu wenye
asili mbalimbali , hivyo kuutambulisha
utamaduni wa Mtanzania.
Kazi na shughuli za Filamu nchini zimekuwa
zikisimamiwa na Sera ya Utamaduni ambayo
ilitayarishwa na kupitishwa mwaka 1997
pamoja na Sheria ya Filamu na Michezo ya
Kuigiza na 4 ya mwaka 1976.
Katika kipindi cha kuanzia mwaka 1997
hadi mwaka 2013 kumekuwepo na maendeleo
makubwa katika Tasnia ya Filamu nchini
hivyo kuisababishia Sera ya Utamaduni ya
Mwaka 1997 kutokidhi baadhi ya mahitaji
ya tasnia ya filamu na kupelekea mahitaji
ya kurekebisha Sera ya Utamaduni kama
Sera mama na kutungwa kwa Sera ya
Filamu.
Mnamo Desemba 12 mwaka 2013, wadau
mbalimbali kutoka Wizara ya Habari , Vijana
Utamaduni na Michezo , Bodi ya Filamu,
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa
Umma, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya
Ufundi na Wizara ya Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi walishiriki katika
kikao cha wadau cha kujadili rasimu ya
awali ya Sera ya Filamu.
Wadau wengine ni Wizara ya Afya na Ustawi
wa Jamii , Wizara ya Kazi na Ajira, BASATA,
Idara ya Sanaa na Sanaa za Maonyesho ,
Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam, Mamlaka ya
Mapato Tanzania, Mtandao wa Muziki,
Swahili Films , ROSAF , TAPAF , Umoja wa
Mashirikiano wa Filamu, Filamu Cental ,
Chama cha Hakimiliki Tanzania, Shirikisho
la Sanaa za Maonyesho pamoja na G & S
Associates and Advocates.
Hata hivyo wadau ambao hawakushiriki
walipewa nafasi na Serikali kuwasilisha
maoni yao ambapo mwitiko umekuwa mzuri
na maoni yanaendelea kupokelewa ili
hatimaye kuwa na Sera bora na shirikishi .
Katika kikao hicho Rasimu ya awali ya Sera
ya Filamu iliwasilishwa kwa kuelezea historia
fupi ya filamu nchini, vikao vya wadau
vilivyofanyika vya mapendekezo ya kuwa na
Sera ya Filamu kati ya mwaka 2004 na 2013,
nyaraka kama Mpango Mkakati wa Bodi ya
Filamu unaoonyesha haja ya kuwa na Sera
ya filamu pamoja na kuelezea malengo
mahususi na matamko ya Sera mpya
inayopendekezwa kutungwa .
Aidha , wadau walijadili uzoefu wa nchi
nyingine kama Kenya, Nigeria, China,
Afrika Kusini , Marekani , Canada , India na
Uingereza na matokeo ya tafiti mbalimbali
zilizofanyika pamoja na Changamoto
zinazoikabili Tasnia ya Filamu nchini.
Miongoni mwa mapendekezo yaliyotolewa na
wadau ni pamoja na kuwa Sera itamke
uanzishwaji wa Chuo cha Taifa cha Filamu ,
Sera itamke kuwepo kwa Mfuko ambao
utasaidia katika kuimarisha Sekta ya
Filamu na Sanaa za maonyesho kwa ujumla,
Sera itoe tamko kuhusu kusimamia maadili
katika tasnia ya Filamu na kudhibiti
ukatili wa kijinsia katika tasnia ya Filamu.
Pia walipendekeza kuwa hoja na matamko
yawe na takwimu zaidi , Sera itamke namna
ya kumlinda msanii wa Tanzania ,
mzalishaji wa ndani na wawekezaji, pamoja
na kupiga vita udhalilishaji wa watoto wa
kike.
Kwa upande mwingine, wadau hao walitoa
pongezi kwa Wizara kwa kuandaa Rasimu ya
awali ya Sera ya Filamu iliyotokana na
maoni mbalimbali ya wadau , Sera ambayo
itaiwezesha Tasnia ya Filamu kupata
mwelekeo bayana na kukidhi matakwa ya
kila mdau katika tasnia ya filamu .
Wizara inapenda kuujulisha umma kuwa
imekua na inaendelea kushirikiana na
wadau wa Filamu kwa kila hatua ili
hatimaye ifanikishe azma ya kuwa na
nyaraka zote muhimu katika kuendeleza,
kusimamia , kuratibu na kukuza tasnia ya
filamu nchini.

Sunday, March 9, 2014

JAMAA TULIYEMREPORT KUWA ANATONGOZA WATU WHATSAPP KUMBE NI SHOGA!

Jamaa aliyejifanya msichana na kuanza kusumbua watu kwenye whatsapp amegundulika ni shoga sababu amekuwa akiwapigia simu hovyo wanaume wenzie akiwataka waonane nae waongee biashara,kana kwamba haitoshi akatoa na namba yake ingine ambayo imesajiliwa kwa jina la FADHILI
MTENGE

NAMBA ZAKE HIZO NI 0715 952 856
+255 776 326 079
Hiyo ya zantel ukimchek whatsapp utampata!

Picha anazoweka profile picha ni hizi zifuatazo

Kama picha zinazotumika ni zako unaombwa kureport police haraka iwezekanavyo

KUNA MVULANA ANAJIFANYA MSICHANA MSAGAJI AMEKUWA AKITONGOZA WATU WATSAPP

Huyo kaka amekuwa akijifanya msichana msagaji na amekuwa akitumia picha ya mdada kujifanya ni yeye mmoja wa waliotumiwa sms na huyu kaka ameshareport police na hiyo namba tigo washaombwa waifatilie pia police wanafatilia mwenye hizo picha za msichana uchunguzi ukikamilika tutaweka namba

Tuesday, March 4, 2014

ABIRIA AJICHINJA NDANI YA BASI


Makongoro Oging’ na Haruni Sanchawa
AMA kweli duniani kuna mambo kwani
dereva na abiria wa basi la Manchester
ambalo namba yake haikujulikana mara
moja , lililokua likitoka Lindi kwenda jijini
Dar es Salaam walijikuta wakiangua vilio
baada ya kumuona mwenzao akijichinja
hadi kufa kwa kisu ndani ya gari hilo .
Ujumbe kabla ya kifo : Kijana aliyejichinja
ndani ya basi akiandika ujumbe kabla ya
kukata roho.
Kwa mujibu wa chanzo, tukio hilo la
kusikitisha lilitokea saa tisa alasiri,
Jumatano wiki iliyopita mara basi hilo
lilipofika katika hoteli moja ya Nangulukulu
kwa ajili ya kupatia chakula.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na
waandishi wa habari hii jijini Dar es Salaam
mwishoni mwa wiki iliyopita, baadhi ya
abiria walioshuhudia tukio hilo walisema
kuwa mara walipofika katika hoteli hiyo ,
kila mmoja alitawanyika kwa lengo la
kujipatia chakula na baadhi yao walienda
maliwatoni akiwemo marehemu huyo .
Msaada: . ..Kijana huyo akitolewa kwenye
basi baada ya kujichinja kwa sime.
Walisema kwamba marehemu huyo ambaye
jina lake halikupatikana mara moja ,
wakati wa kushuka hakuonekana na kisu
aina ya sime lakini baadaye abiria
wachache waliotangulia kwenye gari ,
walimshuhudia akiwa ameshika sime hiyo
mkono pasipokujua aliipata wapi.
“Hata sisi tulishangaa kumuona akiwa
karibu na usukani wa dereva huku
akizamisha sime tumboni kisha kuichomoa
na kujichinja shingoni hadi pale alipokuwa
akivuta koromeo na kuning’ inia .
Damu kila mahali : . .. Akiingizwa katika gari
lingine huku damu zikiwa zimetapakaa.
“Tulichanaganyikiwa kwani ni kitu ambacho
hatukukitarajia na wala hatujawahi
kushuhudia tukio kama hilo la mtu
kujichinja hadharani , tulibakia kutokwa
machozi huku akina mama wakipiga yowe ,
hakuna mtu aliyethubutu kumsogelea
kumuokoa kwani kila mmoja alimuogopa.
“Tulishindwa kupanda basi hilo kwani ni
tukio la ajabu pia ndani kwa mbele
kulikuwa kumetapakaa damu , ghafla
alidondoka chini ndani ya gari , aliomba
kalamu na karatasi ili kuandika ujumbe.
Silaha: Polisi akiwa na sime aliyotumia
kujichinja kijana huyo .
“Dereva alichukua kalamu na kipande cha
karatasi na kumpa , alianza kuandika huku
damu ikimbubujika tumboni na shingoni,
hatukujua alichokiandika , aliishiwa nguvu
taratibu akadondoka .
“Abiria walimsogelea na kumuinua na
walimueleza kuwa atubu kwa Mungu kosa
alilolifanya kabla hajafa , alipiga magoti
na kuomba, ghafla alidondoka tena .
Imani: Kijana akisali kabla ya kukata roho.
“Kaka yake ambaye alikuwa akisafiri naye
kuelekea Dar es Salaam alichanganyikiwa
kwani hakutegemea kuwa mdogo wake
angejiua , kwani alisema hana historia ya
kuugua ugonjwa wa akili. Polisi walipigiwa
simu na walifika kumchukua lakini baada
ya muda mfupi akawa amefariki dunia .
“Sisi abiria wengine tuliendelea na safari
kuelekea Dar es Salaam ambapo marehemu
na kaka yake walibakia huko mkoani Lindi .
Kifo: .. .Kijana huyo baada ya kukata roho.
“Mara tulipofika Dar es Salaam dereva
alitusihi tukae kimya kwa dakika moja na
kuomba kutokana na tukio lililotupata,
tulifanya hivyo baadaye kila mmoja
alitawanyika na kuelekea kwake, ” kilisema
chanzo kwa sharti la kutoandikwa jina
gazetini .
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi , ACP
Renatha Mzinga alipoulizwa mwishoni mwa
wiki iliyopita kuhusiana na tukio hilo alikiri
kutokea.
“Ni kweli tukio hilo lilitokea lakini kwa sasa
sina data kwani nipo njiani nikitokea
Nairobi, Kenya kikazi kuelekea Lindi , mara
nitakapofika huko ofisini ndipo nitapata
tukio zima lilivyokuwa, ” alisema Kamanda
Mzinga.

BILIONEA ANASWA KWA UNGA DAR


BILIONEA maarufu jijini Dar es Salaam , Ali
Khatibu Haji ‘Shkuba’( 44 ) ambaye alikuwa
akisakwa kwa muda mrefu na Kikosi
Maalum cha Polisi Tanzania kwa madai ya
kujihusisha na biashara haramu ya ‘unga ’,
amenaswa.
Bilionea Ali Khatibu Haji ‘Shkuba’( 44 )
aliyenaswa na polisi .
Vyanzo vililiambia gazeti hili kwamba ,
mtuhumiwa huyo alikamatwa Uwanja wa
Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere
(JNIA ) jijini Dar, Februari 23, mwaka huu ,
saa sita mchana akijianda kwenda nchini
Afrika Kusini .
Kwa mujibu wa chanzo hicho , mara baada
ya Shkuba kukamatwa alisafirishwa usiku
huohuo kwenda mkoani Lindi chini ya ulinzi
mkali wa polisi ambapo Februari 27 , mwaka
huu aliunganishwa na watuhumiwa wengine
na kufikishwa katika Mahakama Kuu Kanda
ya Kusini .
Madawa ya kulevya .
Shkuba ambaye ni mkazi wa Mikocheni , Dar
ni mfanyabiashara mwenye maduka ya
kubadili fedha (bureau de change) jijini,
ana makampuni ya ulinzi na nyumba
Mikocheni pia anamiliki magari ya kifahari
likiwemo aina ya Jeep lenye thamani ya
zaidi ya shilingi milioni 150.
Vyanzo hivyo vilisema mtuhumiwa huyo
alikuwa akisakwa na kikosi kazi tangu
Januari 12 , 2012 na inadaiwa kwamba
alikimbilia nje ya nchi na kurudi kwa siri
na ndipo jeshi hilo liliamua kumuwekea
mtego.
Taarifa ziliendelea kusema kuwa, tangu
vita ya kuididimiza biashara ya unga ianze
nchini, hakuna bilionea aliyewahi
kukamatwa zaidi ya mtuhumiwa huyo .
Gari aina ya Jeep lenye thamani ya zaidi
ya milioni 150 ambalo ni mojawapo ya
magari ya kifahari anayomiliki Shkuba.
Vyanzo vingine vya habari toka ndani ya
jeshi hilo vinadai kwamba, Shkuba aliwahi
kukamatwa mwaka 2006 kwa kuhusishwa na
biashara hiyo haramu na kuwekewa ulinzi
wa kifungo cha nje .
Habari zinadai kuwa, Januari 12 , 2012,
kikosi kazi cha kupambana na biashara hiyo
kilipata taarifa ya kuwepo kwa madawa
hayo aina ya heroin kiasi cha kilo 211 yenye
thamani ya shilingi bilioni 9 .4 mkoani Lindi
yakiwa tayari kusafirishwa nje ya nchi .
Kikosi hicho kiliweka mtego maeneo ya
Machinga Two mkoani humo na kufanikiwa
kukamata unga huo uliokuwa umefichwa
katika hoteli moja .
Binti wa Liyumba, Maureen Liyumba, siku
alipokamatwa pamoja na wenzake wakiwa
na madawa ya kulevya yenye thamani ya
shilingi bilioni 9 . 4 mkoani Lindi yakiwa
tayari kusafirishwa nje ya nchi.
Watu wanne walikamatwa sanjari nao ,
akiwemo binti wa aliyekuwa Mkurugenzi wa
Utumishi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ,
Amatus Liyumba, Maureen Liyumba ambaye
yuko mahabusu mpaka sasa na ameungana
na Shkuba.
Vyanzo hivyo vilidai kwamba watu hao
walikuwa wakiwasiliana na Shkuba ambaye
watuhumiwa walimtaja na ndipo polisi
walipoanza kumfuatilia .
Madawa ya kulevya aliyokamatwa nayo
binti wa Liyumba na wenzake .
Siku moja nusura polisi wamkamate ambapo
alikimbia na kulitelekeza gari lake aina ya
Toyota Land Cruiser lenye namba za usajili
T 921 BPY ambalo bado linashikiliwa katika
Kituo Kikuu cha Polisi Mkoa wa Lindi .
Inadaiwa kwamba polisi walipokwenda
nyumbani kwake jijini Dar walimkosa na
kila walipopiga simu zake zilikuwa
hazipatikani hewani lakini baada ya
kumkamata walimpeleka Lindi kwa
helikopta .
Kamanda wa Polisi Kikosi cha Kudhibiti na
Kupambana na Madawa ya Kulevya
Tanzania, SACP Godfrey Nzowa alipoulizwa
juzi na Uwazi kuhusu madai hayo
alithibitisha kukamatwa kwa Shkuba na
kwamba tayari ameunganishwa na wenzake
mkoani Lindi na wanaendelea kuwasaka
mabilionea wengine ndani na nje ya nje ya
nchi.
Maureen Liyumba pamoja na watuhumiwa
wenzake .
“Ni kweli tulikuwa tukimsaka kwa muda
mrefu Bwana Shkuba na tulijipanga vizuri
sisi kikosi kazi hali iliyotufanya tumnase .
“Hii vita ya biashara haramu kwa sasa si
kwa Tanzania tu bali ni vita ya dunia
nzima, nawaomba wananchi wazidi kutupa
ushirikiano na tutayafanyia kazi kwa siri
maelezo yao, ” alisema Kamanda Nzowa .

MASKINI JACK HALI MBAYA

MODO mwenye mvuto Bongo Jacqueline
Patrick ‘ Jack ’, ambaye yuko mahabusu ya
Gereza la Qincheng nchini China kwa madai
ya kunaswa na madawa ya kulevya nchini
humo, anazidi kuteseka , safari hii akidaiwa
kukabiliwa na tatizo kubwa la kiafya .
Jacqueline Patrick ‘Jack ’ .
Kwa mujibu wa chanzo chetu , Jack
anasumbuliwa na ugonjwa wa kukosa hamu
ya kula, hali iliyomfanya apoteze uzito wa
kilo kumi huku akikabiliwa na tatizo lingine
la kupungua kwa kasi ya mapigo ya moyo .
KAMA HALI ITAENDELEA
Chanzo kimesema kuwa endapo hali ya
kuzorota kwa afya hiyo kutaendelea, Jack
anaweza kujikuta katika tatizo kubwa zaidi
ambalo linaweza kusumbua kwenye
mwenendo mzima wa kesi yake.
“Kusema kweli kuhusu maisha ya mahabusu
si mabaya sana kwake, hateswi kwa kupigwa
wala hanyimwi chakula, ila hana uhuru
binafsi, ni kama amefichwa , naamini
matatizo hayo ya kiafya yanatokana na
uzito wa kesi yake , ” kilisema chanzo hicho .
MLOLONGO WA MAMBO
Habari zaidi zinadai kwamba kesi ya msingi
ya staa huyo kudaiwa kukutwa na madawa
ya kulevya itaanza kusikilizwa rasmi
Septemba, mwaka huu baada ya
mwanasheria wake kukamilisha taratibu
zote.
“Ile kesi yake sasa ni Septemba mwaka huu .
Si unajua hajawahi kupandishwa kizimbani
kuulizwa kama ni kweli alikamatwa na unga
au la !” kilisema chanzo hicho .
Jack Patrick akiwa amefunikwa uso baada
ya kukutwa na pipi za heroin tumboni nchini
China.
WAKILI WAKE ANATOKA HONG KONG
Taarifa zaidi zinasema kuwa wakili wa
mrembo huyo anatoka jijini Hong Kong
nchini humo ambako ndiko kwenye
wanasheria wazuri kwa kiwango cha kesi
yake ya unga .
KUMWONA NI KWA AHADI
Ikazidi kudaiwa kwamba kuna Mtanzania
mmoja tu ambaye amekuwa na fursa ya
kumuona modo huyo na kabla ya kwenda
lazima aombe na kupewa ‘apointimenti ’
maalum.
WALIOMTUMA WAMPIGA CHENGA , WALA
‘BATA’
Tofauti na kwa Video Queen wa Bongo,
Agnes Gerald ‘Masogange’ ambaye naye
aliwahi kupata msala mkubwa kama huo
nchini Afrika Kusini , Julai , mwaka jana
ambapo ‘mabosi ’ wake walikuwa mstari wa
mbele kumhangaikia , Jack anasota
mwenyewe.
Habari zinasema kuwa hakuna cheni yoyote
kutoka kwa watu ambao wanatafsiriwa kuwa
ni waliomtuma kwani wanaosumbuka ni watu
wake wa karibu, wakiwemo ndugu zake .
Juzi , Risasi Mchanganyiko lilizungumza na
mtu wa karibu sana na mtuhumiwa huyo
ambapo alikiri Jack kuwa na hali ngumu
katika kesi yake hiyo huku akisema kwamba
watu wanaodaiwa ndiyo mabosi wake
wanakula ‘bata ’ tu jijini Dar es Salaam .
“Unajua tatizo la biashara ya unga ni hapo
tu! Wewe unayebeba ukinaswa ni juu yako,
waliokutuma wao wanachofanya ni
kuthibitisha tu kuwa ni kweli umekamatwa
maana wapo wanaodaiwa wamekamatwa
kumbe si kweli , wanaingia mitini na mzigo , ”
alisema mtu huyo .
SABABU ZA MOYO KUSHINDWA KUSUKUMA
DAMU
Juzi , gazeti hili lilimtafuta daktari mmoja
wa Hospitali ya Taifa Muhimbili ( jina lipo )
na kumuuliza tatizo la moyo kushindwa
kusukuma damu ambapo alisema:
“Moyo kushindwa kusukuma damu kwa
mwendo wa kawaida husababishwa na
shinikizo la damu lisilodhibitiwa, mgonjwa
kushindwa kudumisha udhibiti wa maji
mwilini, chakula au dawa.
“Sababu nyingine ni upungufu wa damu na
utoaji wa kiwango cha juu cha homoni za
koromeo ambazo zinaleta maumivu ya ziada
kwenye misuli ya moyo , utumiaji mwingi wa
vimiminika au ulaji wa chumvi uliopitiliza
na utumiaji wa dawa ambazo husababisha
uwekaji wa maji mwilini kama vile
Hiazolidinedione.”
KUHUSU KUKOSA HAMU YA KULA
Kwa mujibu wa daktari huyo , tatizo hilo
humkumba mtu anapokuwa katika msongo
mkubwa wa mawazo kutokana na jambo zito
linalomkabili , ambalo halina mlango wa
kutokea.
TUKUMBUKE
Mrembo huyo alikamatwa Desemba 19 ,
mwaka jana katika Uwanja wa Ndege wa
Macau, China akitokea Bangkok , Thailand
akiwa na kete 57 ( kilo 1 . 1 ) za heroin
tumboni zikiwa na thamani ya jumla ya
zaidi ya shilingi milioni 300.
Awali ilidaiwa kuwa kesi yake ingeanza
kusikilizwa mwaka 2016 baada ya yeye
kujifunza Kireno ( lugha inayotumika
Macau) kwa miaka miwili .

Monday, March 3, 2014

MWEE! ETI KISA CHA KAJALA KULISHWA SUMU NI MUME WA MTU


Wiki iliyopita muigizaji wa filamu nchini Kajala
Masanja alikiri kuwekewa sumu wakati
alipokuwa kwenye show ya mwanamuziki Izzo
Buzness. Star huyo aliwahi hospitalini na hali
yake kuwa nzuri. Hata hivyo star mmoja wa
filamu akizungumza na Swahiliworldplanet kwa
sharti la kutoandikwa jina lake alisema kuwa
Kajala alifanyiwa kitendo hicho cha kifedhuli
kutokana na madai ya kutembea na mume wa
mtu ambaye anadaiwa kumpangishia nyumba
ya kifahari "kachukua mume wa mtu huyo
Kajala, yes kuna libaba limempangia nyumba
nzima so nahisi ndiyo sababu ya kuwekewa
sumu" kilisema chanzo hicho.
Hata hivyo Kajala alijaribu kutafutwa ili
kutolea ufafanuzi madai hayo lakini kwa siku
mbili hakuweza kupatikana.

.